Breaking News

WATANZANIA WAJITIKEZA KUMSHANGILIA SAMMATA



Wadau wa sekta ya Utalii kutoka Tanzania, Tim Mdinka na Eugen Malle jana walikuwepo uwanja wa Luminus Arena (uwanja wa nyumbani wa KRC Genk) wakimshuhudia Samatta akifanya yake kwenye mchezo wa ligi kati ya Genk na Standard Liege.

Katika mchezo huo, Samatta alifunga mabao mawili, baada ya game walipata fursa ya kuzungumza nae kwa kifupi ikiwa ni pamoja na kumpongeza Samatta na kupiga picha kwa ajili ya ukumbusho.

“Tuliuteka uwanja jana na bendera zetu za Tanzania, leo story ndio hiyo mji mzima. Dogo alitupa burudani ya kutosha jana”-anasema Tim Mdinka, moja ya wadau wa utalii.

“Tulipata muda wa kumpongeza alipo maliza interview baada ya mechi”.

No comments