MPAPASO NJE NDANI WAENDELEA YANGA SAFARI:- SPORTPESA
Kikosi cha Yanga kimeondoshwa katika mashindano ya SportPesa Super Cup kwa kukubali kipigo cha mabao 3-1 dhidi ya Kakamega HomeBoys, mchezo uliopigwa mjini Nakuru, Kenya.
Kakamega wamejipatia mabao yao kupitia kwa Allan Wanga aliyefunga mawili huku moja likiwekwa kimiani na Opondo. Bao pekee la Yanga limewekwa kiminiani na Matheo Anthony kwa njia ya mpira wa faulo.
Matokeo hayo yanaibakiza Kakamega huku Yanga ikiyaaga rasmi mashindano na jumla ya timu nne kutoka Tanzania ambazo ni JKU, Singida United na Simba Sc zikisalia.
Muda mchache kuanzia sasa JKU kutoka Zanzibar itakuwa inakipiga na na mabingwa wa Ligi Kuu Kenya msimu uliomalizika, GorMahia FC.
No comments