Breaking News

SIMBA MSHINDI WA TATU SPORTPESA, AMFUNGA MBAO UWANJA WA TAIFA





MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara Simba, leo wameibuka washindi wa tatu katika mchezo wa SportPesa Cup Uwanja wa Taifa kwa kushinda mbele ya Mbao kwa penalti 5-3.

Dakika 90 za mchezo huu ambao ulikuwa na kasi kwa timu zote mashabiki walishuhudia timu zikitoka suluhu na kupelekea mwamuzi kuamua ipigwe mikwaju ya penalti.

Simba walifunga penalti zote tano huku wapigaji wakiwa ni Emanuel Okwi, Pascal Wawa, Deogratius Munish, Nicholas Gyan na Clatous Chama.

Kwa upande wa Mbao waliofunga walikuwa ni Said Khamis, Vincent Philipo na Peter Mwangosi huku Rajesh Kotecha akikosa penalti ya nne.

Kwa matokeo hayo Simba wanakuwa washindi wa tatu wa mashindano ya SportPesa Cup huku Mbao wakishika nafasi ya nne.


1 comment:

  1. I like viewing web sites which comprehend the price of delivering the excellent useful resource free of charge. I truly adored reading your posting. Thank you! How to connect to your tattoo artist

    ReplyDelete